Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara amefanya ziara katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere huku akiutaka uongozi wa uwanja huo kuboresha mapungufu waliyonayo ikiwemo suala la kuwasiliana na idara nyingine. Mbali na hilo pia Waitara amezungumzia suala la ratiba za ndege kutoeleweka na uwanja wa ndege alioukuta hauna umeme.