Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi,
Israeli na aseme sasa, -
2 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi,
Wanadamu walipotushambulia.
3 Papo hapo wangalitumeza hai,
Hasira yao ilipowaka juu yetu -
4 Papo hapo maji yangalitugharikisha,
Mto ungalipita juu ya roho zetu;
5 Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu
Maji yafurikayo.
6 Na ahimidiwe Bwana;
Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao.
7 Nafsi yetu imeokoka kama ndege
Katika mtego wa wawindaji,
Mtego umevunjika, nasi tumeokoka.
8 Msaada wetu u katika jina la Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi.